Uchaguzi wa Tanzania 2020: Mahakama ya Afrika yataka Tanzania kuruhusu kupingwa kwa matokeo ya urais mahakamani
Mahakama ya tanzania hairuhusu matokeo ya uchaguzi kupingwa mahakamani
Mahakama ya Afrika imeamuru Tanzania kuviruhusu vyama vya siasa kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais mahakamani
Katiba ya Tanzania hairuhusu mahakama kuhoji wala kupinga matokeo ya urais mara mshindi wa uchaguzi atakapokuwa ametangazwa na tume ya uchaguzi
Lakini jana, Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, yenye makao yake makuu jijini Arusha, Kaskazini mwa Tanzania, imeitaka Tanzania kuchukua hatua "za muhimu za kikatiba na za kisheria, ndani ya muda mwafaka" kubadilisha sheria hiyo inayozuia kupingwa kwa matokeo ya urais
Kesi hii ilipelekwa mahakamani hapo na Mtanzania na mwanasheria nguli wa haki za binadamu Jebra Kambole ambaye alihoji kwamba kifungu hicho cha sheria kinachozuia kupingwa kwa matokeo ya uchaguzi wa urais kinakiuka haki zake za msingi
Uamuzi huu wa mahakama ya Afrika unakuja wakati ambao matokeo ya uchaguzi wa urais ya nchi za jirani za Kenya na Malawi yalipingwa mahakamani na mahakama kuamuru marudio ya chaguzi hizo
Wakati marudio ya uchaguzi wa nchini Kenya yalisusiwa na vyama vya upinzani nchini humo, kurudiwa kwa uchaguzi nchini Malawi kulipelekea muungano wa vyama vya upinzani kushinda
Hata hivyo kutokana na siku chache kubakia hadi uchaguzi mkuu kufanyika, kuna uwezekano mdogo wa mabadiliko hayo kufanyika juu ya uchaguzi wa mwaka huu
Hii ina maana gani kwa raia wa Tanzania?
Mwanasheria Jebra Kambole ambaye ndiye aliyepeleka shauri hilo mahajamani amesema;
''Uamuzi huu una maana kubwa sana kwa Watanzania, kwanza kabisa lilikua suala la muda mrefu kwamba matokeo ya urais yanaweza kupingwa mahakamani au la.
Ni jambo ambalo limekuwa likipigiwa kelele kwa muda mrefu sana kwa hiyo ina maanisha kuwa watu wataweza kuyapinga matokeo ya urais mahakamani ambapo kabla ya uamuzi huu mahakama ilikuwa haiwezi kusikiliza jambo lolote ambalo linahusiana na uchaguzi wa urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
''Hivyo ina maana kuwa haki za msingi za Watanzania zinaanza kuonesha mwanga na zi

Comments
Post a Comment